Breaking News

Thursday, February 27, 2014

MAOMBI KWA AJILI YA KIONGOZI WA MAONO

Matendo 12: 5, ukisoma huu mstari wa tano utaona umuhimu wa kuombea kiongozi wa maono kama ambavyo kanisa lilimuombea Petro na akafunguliwa katika vifungo vyake.

KWANINI TUOMBE KWA JUHUDI KWA AJILI YA KIONGOZI?

Kwasababu  kuna mambo mengi ambayo anakutana nayo ambayo hawezi  kuyashinda peke yake lazima tuwe wengi tunayesimama naye, soma  Kutoka  17:11-13 , ukisoma habari hii utaona jinsi ambavyo

Musa aliponyanyua mikono peke yake alichoka na alipochoka walishindwa vita, lakini Haruni na Huri walipomsaidia walishinda vita.

Elewa kuwa kazi ya kumuombea mchungaji kiongozi sio ya

watu fulani, ni yako wewe pia. Acha kuangalia watu wengine fanya wewe kama vile hakuna mtu mwingine. Jambo hili liwe sehemu ya maisha yako ya kila siku

No comments:

Post a Comment

Featured Post

UNAITUMIAJE NAFASI ULIYONAYO?

Kufanikiwa kwako katika maombi kunategemea unavyoitumia nafasi yako uliyonayo katika ulimwengu wa Roho. Jadili

Breaking News