Soma : 1Yohana 4:7
Wapenzi na tupendane kwa kuwa pendo
latoka kwa Mung na kila apendaye amezaliwa na Mungu naye anamjua Mungu.
A. Tuombee Taifa letu la Tanzania mbele za Mungu, Watanzania
wote wapewe pendo la Mungu katika maisha yao waweze kupendana kama ndugu.
Omba upendo wa Mungu uweze kufuta :-
Ubaguzi wa rangi na tofauti za kijinsia
B.Tuwaombee Watanzania wote
wamilikiwe na upendo wa Mungu katika imani zao, katika elimu zao, biashara zao na tabaia zao za asili
au tabia zao za kidini ,upendo upate kuwaongoza.
1Yohana 4:21 "Na amri hii tumepewa na yeye ya kwamba yeye ampendaye Mungu ampenda na ndugu yake". Tuombee watanzania wote wanaoamini katika dini mbalimbali zinazomkiri Mungu wapokee amri hii kuwa upendo wao kwa Mungu wauonyeshe kwa kuwapenda ndugu zao.
No comments:
Post a Comment