Kusamehe huachilia wokovu katika maisha yetu, ndio maana asiyeweza kusamehe naye hatasamehewa na Mungu Mathayo 6: 15.
MAOMBI
- Omba : Mungu nisamehe makosa yangu yote niliyokukosea kwa kuwazia, kuwatendea na kuwanenea vibaya wale wote walionikosea.
- Omba : Mungu nisaidie niweze kusamehe saba mara sabini (Mathayo 18:21-22)
- Omba : Mungu nisaidie kila nisimamapo kusali kwanza nisamehe walionikosea(Marko 11: 25)
- Omba: Mungu nisaidie niweze kuchukuliana na kusamehe( wakolosai 3: 13)
- Omba: Mungu nisamehe na roho ya uchungu inayosababishwa na kutokusamehe.
- Omba : Mungu nisaidie kuwa mtu ninayesamehe ili majeraha ya ndani yasiwepo katika maisha yangu.
MUNGU AKUBARIKI
No comments:
Post a Comment